Friday, August 10, 2012

MAADUI na MWOKOZI


 Kumwamini yesu kristu kama mfalme na mwokozi wetu hakutaweza kutatua matatizo yetu yote,japo tutapata nguvu ya kiroho itakayotusaidia kupambana na matatizo hayo tuwapo hapa duniani,sote twatambua kuwa hatuwezi tukaishi katika dunia hii bila dhambi kwani ni Kristu pekee aliyeishi maisha bila dhambi pengine tujiulize ni kwa nini wanadamu tunatenda dhambi ili hali tunaelewa wazi kuwa Mungu anachukia dhambi.....?Jibu ni kwamba kuna maadui watatu ambao husababisha tumkosee muumba wetu,nao ni hawa wafuatao.
          
         SHETANI....Baadaa ya kutupwa duniani,shetani aliapa kutukosanisha sisi wanadamu na Mungu hivyo hutumia kila mbinu kutushawishi ili tutende dhambi,mbinu yake kuu ni uongo na hufanya kila njia ili kufanya mwanadamu asitambue baraka alizonazo kutoka kwa Mungu,shetani hututia huzuni,wasiwasi,woga,hofu ili tusiutazame utukufu wa Mungu,pia hutujaza tamaa,wivu,chuki,hasira ili tumkosee Mungu na wanadamu wenzetu.

          DUNIA.....Maisha tunayoishi katika dunia hii iliyomuasi Mungu hayatoweza kumpendeza Mungu....Binadamu na tabia zetu,utaratibu wa mambo ya kidunia na vishawishi vyake hutufanya tuishi ya dhambi na kumchukiza Mwenyezi Mungu.Maandiko yanasema "kupenda ya dunia ni uadui na Mungu"...mambo mengi yanayochukuliwa kama mambo ya  kisasa hupelekea kila mmoja wetu kunaswa katika dhambi mfano,mavazi yasiyofaa,filamu chafu,tamaa iliyokithiri ya pesa na madaraka,uchawi na nguvu za giza vyote hivi na vingine vingi hutuweka katika gereza la dhambi.

         MIILI YETU.......Mungu alituumba kwa mfano wa sura yake ili ajitukuze kupitia maisha yetu yakumpendeza tutakayoishi katika hii dunia kabla hajatuchukua na kutushirikisha katika maisha ya milele huko mbinguni,alitupa viungo mbali mbali na akaweka utaratibu wa namna ya kuvitumia kwani alijua wazi bila utaratibu huo tutapotoka...bahati mbaya miili hii ambayo ni hekaru la Roho mtakatifu tunaitumia vibaya kwa dhambi,mfano ulevi wa pombe,uzinzi,mauaji na anasa za dunia,maanndiko yanasema "hakika roho i tayari bali mwili hau tayari" ni kweli miili yetu inapingana na mapenzi ya mungu japo roho zetu zinampenda au la!

         maandiko yanasema "mshahara wa dhambi ni mauti" ni kweli kwamba kwa wenye dhambi wataishia jehanamu na walio okoka watakwenda mbinguni......"Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa mwanae wa pekee ili atukomboe sisi wanadamu"ni kweli kwamba kutaka kuwa watakatifu katika dunia hii,na shetani akitupotosha huku miili yetu wenyewe inapenda anasa za dunia isingewezekana hivyo Mungu akamtuma mwane wa pekee aje atukomboe.

       YESU KRISTU........Wokovu ni bure na yeyote atakaye mpokea na kumwamini yesu kristu kama mwokozi na mfalme wake na kwamba alipokwenda msalabani alilipa dhambi zake,hakika ataishi milele...