Miongoni mwa wafuasi vipenzi wa Yesu,alikuwa mtu mmoja aitwae Lazaro,mwenyeji wa Bethani....Lazaro alikuwa anampenda na kumwamini kristu kwani kazi na miujiza aliyokuwa akiitenda ni kielelezo tosha kilichomfanya aamini kuwa neno limekuwa hai na maandiko yalikuwa yanatimia kama jina lake "mungu pamoja nasi" lilivyo basi kristu na maisha yake yote aliyoishi ilikuwa mungu ameamua kujidhihirisha kwa wanadamu ili waweze kumwamini na wapate kukombolewa kutoka katika dhambi iliyokuwa imewafunga na kuwatesa watu wake.
Lazaro alikuwa na dada zake wawili Maria na Martha,hawa pia walimpenda na kumwamini mwokozi vilevile kristu alikuwa anawapenda sana wanandugu hawa na familia yao yote ka ujumla,mara nyingi alipokuwa amechoshwa na kundi kubwa la watu waliokuwa wakimfuata na shida zao hata pale ambapo alizongwa na waliokuwa wanampinga kwa nia ya kumuangamiza kristu alitafuta pumziko katika familia ya wapendwa hawa,hivyo kulikuwa na upendo wa dhati kati yao kama mwokozi na wafuasi wake.
Ghafla siku moja Lazaro alipatwa na ugonjwa mkali hata akawa mahututi kitandani,dada zake,ndugu jamaa na marafiki walikuwa wakijitahidi kufanya kila liwezekanalo ili kuokoa maisha ya mpendwa wao,walijaribu kila tiba na dawa lakini hali yake ilizidi kuwa mbaya.Ilitokea kama maajabu kwamba ndugu hawa wajaribu kumtibu ndugu yao wao wenyewe wakisahau kwamba kwa macho yao walipata kumwona mwana wa mungu akiponya kila aina ya magonjwa.
Baada ya kujaribu kila walichoamini kingeweza kuokoa maisha ya ndugu yao bila mafanikio yoyote,kumbukumbu ilimjia Maria dada yake na Lazaro kwamba kimbilio pekee la suluhisho la kaka yao ni Yesu....Faraja kubwa iliwajaa mioyono mwao baada ya Maria kutoa wazo kwamba upelekwe ujumbe kwa Yesu juu ya hali ya Lazaro,wote walijua jinsi Yesu alivyompenda Lazaro hivyo waliamini mara apatapo ujumbe huo angefika mara moja na kumponya.
Akiwa anaendelea na kazi yake ya kuhubiri injili ya wokovu katika miji mingine kristu pamoja na wanafunzi wake,mara akawajia mtu mmoja akiwa na ujumbe usemao "Bwana,tazama yule umpendae yu mahututi kitandani"...Yesu alipokea ujumbe ule kisha akamuamuru mjumbe aliyeleta habari zile arudi bila kumpa jibu lolote,alipofika Bethani,Maria,Martha watu wote walikuwa wakimngoja kwa shauku wakidhani Yesu angesitisha shughuli zake na kwenda kuwafairiji lakini hawakuamini macho yao walipomwona kwa mbali aliyekuwa amepeleka habari kwa yesu juu ya hali ya rafiki yake kipenzi Lazaro akirejea mnyonge akiwa peke yake bila majibu wala taarifa yoyote,walihuzunika sana lakini ndani ya mioyo yao faraja ya mungu iliwajaa hata hawakumlaumu yesu kwa kutowajali....Baada ya mtu aliyeleta ujumbe kuondoka zake,kristu akawaambia wanafunzi wake
Yesu; "Twendeni katika mji wa Yudea,huko nako tukahubiri injili"
wanafunzi wake walimjua Lazaro na jinsi alivyompenda na kumwamini Yesu hivyo walishamgazwa sana na namna ambavyo yesu alizipokea habari za ugonjwa wake,wakahoji....
Wanafiunzi; "Bwana, tazama yule umpendae yu mahututi kitandani lakini wataka twende Yudea, je umesahau jinsi ambavyo wanakutafuta ili wakuangamize katika mji wa Yudea"?
Yesu; "Siku ina masaa 24,hivyo basi muda wangu pia haujawadia,hamjui ya kwamba mtu hutembea mchana kwani mwanga humwongoza,lakini yule atembeaye katika giza nuru ya mbingu humwongoza?"
Wanafunzi wake walimheshimu Yesu na kuamua kuongozana naye hadi katika mji wa Yuda,huko walikaa kwa takribani siku tatu....Wakati huohuo kule Bethani hali ya lazaro ilizidi kuwa mbaya na hatimaye akafariki.... Dada zake walilia kwa uchungu kwani walimpenda sana kaka yao,mafarisayo na wale waliokuwa wakimpinga Yesu waliwakebehi na kuwacheka chinichini dada wa Lazaro kwa kile ambacho walidai Yesu aliwaterekeza lakini mioyoni mwa Martha na Maria kulikuwa na faraja ya kipekee na waliamua kumwachia na kumtukuza mungu kwani yeye alimpenda zaidi kaka yao.....Baada yataarifa za kifo cha Lazaro kumfikia,Yesu akihubiri injili ghafla akawaita wafuasi wake,akawaambia
Yesu; "jiandaeni twende katika mji wa Bethani nyumbani kwa Lazaro"
Wanafunzi; "Bwana, kuna haja gani ya kwenda ili hali Lazaro amekwisha kufa?"
Yesu; "Ni bora mmejua kuwa amekufa, hii imetokea ili kwa macho yenu mjionee na muweze kuamini"
Safari ilianza kuelekea Bethani,si umbali mrefu sana kutoka walipokuwa na walipokaribia nyumbani kwa Lazaro, Maria aliona kundi la watu likijongea katika msiba huo uliokuwa umejaa watu wengi kwani Lazaro alikuwa mtu maarufu na familia yao ilikuwa na ndugu na jamaa wengi.....tayari maandalizi ya mazishi yalikuwa yamefanyika na mwili wa Lazaro ulikuwa umeoshwa vizuri,umepakwa mafuta na kuvishwa sanda tayari kwa kuzikwa....Maria alipoona kundi lile alijua wazi ni Yesu na wanafunzi wake pamoja na waliomfuata huku na kule,maria alimkimbilia Yesu,alipomfikia akamwangukia miguuni akilia,akasema...
Maria; "Bwana, kama ungekuwapo Lazaro asingekufa"
Yesu; "Usilie, Lazaro hajafa bali amelala tu"
Yesu alipomwambia Maria "Lazaro amelala tu" watu wengi wakiwemo waliokuwa wakimwamini na ambao walikuwa hawamwamini na kumpinga Yesu na kwa masikio yao wenyewe walimsikia yesu akimfariji Maria kwa kumwambia kuwa kaka yao hajafa bali alikuwa amelala tu,Maria alikwenda kumwambia Martha kwamba mwokozi alikuwa amefika kuwafariji na mara baada ya kupata taarifa hizo Martha alifurahi na huzuni yote ilitoweka...Watu wote waliofika msibani pale walitambua kuwa binadamu mwenye nguvu na upendeleo wa mungu alijumuika nao,kwani tangu kristu afike mahala pale utulivu ulitawala,vilio na huzuni viligeuka kuwa nyimbo na mapambio,malaika wa mbinguni walikuwa wametanda katika anga lile na mwili wa Lazaro ulikuwa ndio chombo muhimu ambacho kwa mara nyingine tena Yesu anathibitisha kuwa hakika yeye ni mwana wa mungu....waliomwamini Yesu walikuwa na furaha sana mioyoni mwao kwani walijua wazi nguvu za mbingu zitathibitika tena mahala pale,lakini waliompinga walihofia na kuogopa kwani kadri yesu alivyotenda miujiza watu walimwaini na kumsifu mungu.........Tazama,yesu akasema...
Yesu; "Mmeuweka wapi mwili wa Lazaro?"
Maria; "Ndani ya nyumba hii"
Yesu; "Basi watu wote wakae nje na wachache tuongozane hadi ulipo mwili"
Hapo Yesu,Maria,Martha na watu wazazi wao wakamwongoza kristu hadi mahali ambapo waliulaza mwili wa Lazaro,wakakuta umezungushiwa sanda maalum kwani muda mchache baadae walikuwa wakijiandaa kwenda kuuzika,yesu akasogea karibu na mwili wa Lazaro, akainua kichwa chake juu,akafungua mikono na viganja vyake akamwomba baba yake wa mbinguni kwa dakika chache, kisha kwa sauti kali iliyochoma masikio ya watu wote mahala pale na kupenya katika masikio ya Lazaro aliyekuwa amekufa,akaita..
Yesu; "Lazaro amka!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!"
Taratibu,Lazaro aliyekufa siku tatu kabla,ambaye damu ilisimama kutembea mwilini mwake,ambaye macho yalifumba,masikio yaliziba na pua zake hazikupumua alifumbua macho,masikio yalifunguka,pumzi yake ilirejea na damu ikaanza kutembea mwilini mwake kama mwanzo,akaininuka na yesu akamshika mkono akamwinua na akawaambia watu waliokuwa pale..
Yesu; "mfungueni sanda, mumpatie mavazi yake na chakula ale"
Wakamfungua sanda na kumvisha mavazi safi,Lazaro alionekana mwenye furaha na amani ya mungu ndani yake na Yesu alimkabidhi kwa dada zake Maria na Martha pamoja na wazazi wao.....vilio,huzuni,upweke na nguvu za mwovu vilikuwa historia mahala pale kwani nderemo,vifijo na ufalme wa mungu ulitawala na watu wote walimuamini Yesu na kumtukuza mungu...
Mpendwa,kama hujapokea zawadi ya mungu ya wokovu hujachelewa fanya hivyo sasa kwa kumpokea na kumwamini Yesu kristu kama mfalme na mwokozi wako na mara baada ya kumwamini Yesu,roho mtakatifu atakujia ndani yako ambaye ataishi milele ndani yako na kukuthibitishia ufufuko,wokovu na kukushirikisha katka makazi ya milele huko mbinguni,maandiko yanasema "siku ya mwisho kristu atapaza tarumbeta mawinguni na watu wote wataisikia sauti yake,walio wafu watafufuliwa na kwa wale waliomwamini atawachukua na kwenda nao mbinguni kwa mungu baba,lakini kwa wale wasioamini watakwenda kuzimu...